Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

RUWASA yasaini Mikataba ya Dira za Maji za Malipo Kabla ya Matumizi

RUWASA yasaini Mikataba ya Dira za Maji za Malipo Kabla ya Matumizi

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ameshuhudia zoezi la utiaji saini mikataba ya mradi wa kubuni, kutengeneza na kufunga  Dira za Maji za malipo kabla ya matumizi kati ya RUWASA na Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na DTBi (Dar Teknohama and Business Incubator) wanaoshirikiana na Chuo cha Uhandisi na Ufundi cha Al Maktoum.

Katika awamu ya kwanza taasisi hizo zitatengeneza na kufunga dira 300, baadae mradi huo utapelekwa kwenye maeneo mengi zaidi kulingana na uhitaji.