Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Dira, Dhamira na Tunu za RUWASA

Dira

Kuwa na jamii inayopata huduma ya majisafi, salama na usafi wa mazingira vijijini kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Dhamira

Kutoa na kusimamia huduma ya majisafi na salama na kuhamasisha usafi wa mazingira kwa jamii iishio vijijini kwa ushirikiano, weledi na kwa gharama nafuu.

Tunu za RUWASA

  • Ushirikiano: Kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuhakikisha jamii iishio vijijini inapata huduma ya majisafi na salama;
  • Utu: Kuzingatia utu katika utendaji kazi kwa kuwajali na kuwathamini wateja na wadau wetu;
  • Uwazi: Kutoa huduma kwa wateja wetu kwa kuzingatia ukweli na uwazi;
  • Taaluma na Weledi: Kutekeleza majukumu kwa kuzingatia taaluma na weledi ili kuwa na miradi yenye ubora na endelevu;
  • Uadilifu: Kufanya kazi kwa kuzingatia uadilifu
  • Kuwajibika: Kutekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu  
  • Kujali Mteja: Kuhakikisha mteja anapewa kipaumbele katika utoaji wa huduma
  • Ubunifu: Kuthamini mawazo mapya katika utendaji kazi