Programu ya Malipo kwa Matokeo (PforR) ni mpango
ulianzishwa na Benki ya Dunia (Word Bank) na ulianza Julai 15, 2019 ikiwa ni
sehemu ya program ya uhakika wa usalama wa maji na usafi wa mazingira
vijijini (sub-program under the Sustainable Rural Water Supply and Sanitation
Program – (SRWSP)).
Malengo ya Programu ya Malipo kwa Matokeo (PforR) ni
kuchochea kasi ya utekelezaji wa Mpango wa Uboreshaji Huduma ya Maji na Usafi
wa Mazingira Vijijini kupitia motisha zilizowekwa kwa viashiria ambavyo hupimwa
kupitia mafanikio ya utekelezaji wa kazi mbalimbali kwenye wilaya 86 na mikoa
17 Tanzania Bara.
Program ya Malipo kwa Matokeo (PforR) imesaidi wananchi wa Wilaya ya Kishapu Mkoa wa Shinyanga kupata Huduma ya maji safi na salama
Mwezi Machi, 2023, Mikoa nane (8) ilijumuishwa kwenye
utekelezaji wa Program ya Malipo kwa Matokeo ambapo hapo awali haikuwa sehemu
ya program. Mikoa hiyo ni Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Morogoro, Njombe,
Mbeya na Dodoma. Kwa sasa, program inatekelezwa kwenye Mikoa 25 na Wilaya 137.
Matokeo ya tathmin ya program ya PforR iliyofanyika awamu
ya tatu kuanzia Julai hadi Septemba 2022 imeonesha matokeo chanya ambapo RUWASA
imefanikisha upatikanaji wa zaidi ya shilingi bilioni 377.24 ukilinganisha na
awamu ya pili ambapo matokeo yaliwezesha upatikanaji wa wastani wa
shilingi bilioni 250.
Pamoja na mafanikio hayo yaliyofikiwa wakati wa utekelezaji
wa progamu, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji imedhamiria kuwasilisha
pendekezo la ongezeko la fedha kutoka benki ya dunia kutokana na mafanikio
sambamba na muelekeo wa sekta ya maji na kukabiliana na changamoto
zinazoikabili ya sekta ya maji kwa sasa.
Pamoja na hayo, Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali
ya Tanzania wameandaa ripoti ya mazingira itakayotumika kama mwongozo wakati wa
uandaaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira vijijini pamoja na kutoa
tathmin ya kuelekea uongezwaji wa fedha za miradi. Ripoti hiyo imewekwa wazi
kwa wadau kutoa maoni yao.
Kwa maelezo zaidi, bonyeza hapa chini kupata taarifa zaidi.