HUDUMA
ZA USAMBAZAJI MAJI
Kutokana na Sheria ya
Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Namba 5 ya 2019, RUWASA imepewa jukumu la
kuhakikisha jamii za wananchi waishio maeneo ya vijijini ndani ya Tanzania Bara
zinapata huduma ya maji safi na salama. Hata hivyo, RUWASA inawajibika kutoa
huduma za maji katika maeneo yote ambayo RUWASA itakabidhiwa na Waziri mwenye
dhamana ya sekta ya maji.
Huduma za maji katika maeneo
ya vijijini husimamiwa na kuendeshwa na Jumuiya za Usimamizi wa Huduma za Maji
Ngazi ya Jamii (CBWSO) chini ya usimamizi wa RUWASA katika ngazi ya Wilaya. Ili
kuhakikisha uendelevu wa huduma za usambazaji maji, CBWSO hukusanya tozo za
maji kutoka kwa jamii kama ilivyojadiliwa na kukubaliwa katika vyombo husika.
Aidha, CBWSO inawajibika
katika kufanya matengenezo ya mradi ili kuhakikisha jamii inapata huduma ya
maji safi na salama kila siku.
HUDUMA ZA USAFI WA
MAZINGIRA
RUWASA kwa kushirikiana
na Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu na OR-TAMISEMI kwa pamoja zina jukumu la
kuhakikisha huduma za usafi wa mazingira zinazingatiwa na kutekelezwa katika
maeneo ya vijijini. Hata hivyo, RUWASA inapaswa kuchochea na kuhamasisha jamii
za vijijini kuzingatia usafi wa mazingira pamoja na kulinda na kuhifadhi vyanzo
vya maji.
Wizara ya Maji na RUWASA
zinawajibika kutoa miongozo na kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya huduma za
usafi wa mazingira maeneo ya vijijini.