Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Huduma

HUDUMA ZA USAMBAZAJI MAJI

Kwa mujibu wa Sheria ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Namba 5 ya 2019, RUWASA ina jukumu la kuhakikisha   wananchi waishio maeneo ya vijijini wanapata huduma ya majisafi na salama. Aidha, RUWASA inawajibika kutoa huduma ya maji katika maeneo maalumu ya mijini kwa idhini ya Waziri mwenye dhamana ya sekta ya maji.

Huduma ya maji katika maeneo ya vijijini zinasimamiwa na kuendeshwa na Vyombo vya Utoaji ya Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) chini ya usimamizi wa RUWASA katika ngazi ya Wilaya. Wananchi  huchangia gharama ya uendeshaji na utoaji wa huduma ya maji ili iwe endelevu.

Aidha, CBWSO inawajibika katika kufanya matengenezo ya skimu za maji ili kuhakikisha jamii inapata huduma ya uhakika ya majisafi na salama.


HUDUMA ZA USAFI WA MAZINGIRA

RUWASA kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu na OR-TAMISEMI kwa pamoja zina jukumu la kuhakikisha huduma za usafi wa mazingira zinazingatiwa na kutekelezwa katika maeneo ya vijijini. Hata hivyo, RUWASA inapaswa kuchochea na kuhamasisha jamii za vijijini kuzingatia usafi wa mazingira pamoja na kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji.

Wizara ya Maji na RUWASA zinawajibika kutoa miongozo na kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya huduma za usafi wa mazingira maeneo ya vijijini.