Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Bodi Mpya RUWASA  yazinduliwa

Bodi Mpya RUWASA yazinduliwa

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso amezindua Bodi mpya ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa PSSSF jijini Dodoma Juni 27, 2023.

Bodi hiyo chini ya Mwenyekiti wake Mhandisi Ruth Koya itahudumu kwa miaka mitatu ambapo katika hotuba yake Mhe. Waziri Aweso alisema ana imani kubwa na bodi hiyo kutokana na uzoefu wa wajumbe wake katika sekta yam aji kwa ujumla.

Waziri Aweso pia ‘aliimwagia’ sifa Bodi ya Kwanza ya RUWASA iliyomaliza muda wake chini ya Mwenyekiti wake Prof. Idrissa Mshoro ambayo imehudumu kwa kipindi cha miaka mitatu baada ya kuanzishwa kwa RUWASA, kwa kazi kubwa ya kuiongoza na kuisimamia taasisi katika majukumu ya kusanifu, kujenga, na kutoa huduma ya majisafi kwa wananchi waishio vijijini.