Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Bwawa la Kwekambala - Wakurugenzi Wasaini Mkataba

Bwawa la Kwekambala - Wakurugenzi Wasaini Mkataba

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mhandisi Clement KIVEGALO akisaini mkataba na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa  ajili ya Ujenzi wa Bwawa la Kwekambala. Hafla hiyo imefanyika katika ofisi ya Mkuu  wa Wilaya ya Handeni tarehe 27 Julai, 2021.Ujenzi wa Bwawa la Kwekambala utasaidia kuondoa kwa kiasi kikubwa tatizo la upatikanaji wa majisafi na salama kwa wananchi waishio katika Wilaya ya Handeni.