Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani

Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kinaongozwa na Mkaguzi Mkuu wa ndani na hufanya shughuli zifuatazo:

i)

Kuandaa na kutekeleza Mipango ya kimkakati ya Ukaguzi;

ii)

Kupitia na kuripoti juu ya udhibiti mzuri wa upokeaji, utunzaji na matumizi ya rasilimali zote za kifedha za Wakala;

iii)

Kupitia na kuripoti juu ya kufuata taratibu za kifedha na kiutendaji zilizowekwa katika sheria yoyote au kanuni yoyote au maagizo ya udhibiti wa matumizi ya Wakala; 

iv)

Kupitia na kuripoti juu ya uainishaji sahihi wa mapato na matumizi;

v)

Kubuni taratibu za ukaguzi ii kukidhi Viwango vya Kimataifa;

vi)

Kupitia na kutoa ripoti juu ya umadhubuti na kuaminika kwa taarifa za kifedha na uendeshaji pamoja na kuandaa ripoti za kifedha na nyingine; 

vii)

Kupitia na kutoa ripoti juu ya mifumo iliyotumika kutunza mali, na kuthibitisha uwepo wa mali hizo;

viii)

Kupitia na kuripoti juu ya shughuli au mipango ili kuhakikisha matokeo yanaambatana na malengo;

ix)

Kupitia na kutoa ripoti juu ya majibu ya uongozi kwenye ripoti za ukaguzi wa ndani, na pamoja na kufuatilia na kusaidia menejimenti kusimamia utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na ripoti na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali; 

x)

Kupitia na kutoa ripoti juu ya Wakala;

xi)

Kufanya ukaguzi wa tathmini ya miradi ya maji na usafi wa mazingira vijijini