Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Huduma za Usambazaji Maji

Kwa mujibu wa Sheria ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Namba 5 ya 2019, RUWASA ina jukumu la kuhakikisha   wananchi waishio maeneo ya vijijini wanapata huduma ya majisafi na salama. Aidha, RUWASA inawajibika kutoa huduma ya maji katika maeneo maalumu ya mijini kwa idhini ya Waziri mwenye dhamana ya sekta ya maji.

Huduma za maji katika maeneo ya vijijini zinasimamiwa na kuendeshwa na Vyombo vya Utoaji ya Huduma za Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) chini ya usimamizi wa RUWASA katika ngazi ya Wilaya. Wananchi  huchangia gharama ya uendeshaji na utoaji wa huduma ya maji ili iwe endelevu.

Aidha, CBWSO inawajibika katika kufanya matengenezo ya mradi ili kuhakikisha jamii inapata huduma ya uhakika ya majisafi na salama.