Kwa mujibu wa Sheria ya Usambazaji Maji na Usafi
wa Mazingira Namba 5 ya 2019, RUWASA ina jukumu la kuhakikisha wananchi waishio maeneo ya vijijini wanapata huduma ya
majisafi na salama. Aidha, RUWASA inawajibika kutoa huduma ya maji katika
maeneo maalumu ya mijini kwa idhini ya Waziri mwenye dhamana ya sekta ya
maji.
Huduma za maji katika maeneo ya vijijini zinasimamiwa na kuendeshwa na Vyombo vya Utoaji ya Huduma za Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) chini ya usimamizi wa RUWASA katika ngazi ya Wilaya. Wananchi huchangia gharama ya uendeshaji na utoaji wa huduma ya maji ili iwe endelevu.
Aidha, CBWSO inawajibika katika kufanya
matengenezo ya mradi ili kuhakikisha jamii inapata huduma ya uhakika ya majisafi na
salama.