Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Huduma za Usambazaji Maji

Kutokana na Sheria ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Namba 5 ya 2019, RUWASA imepewa jukumu la kuhakikisha jamii za wananchi waishio maeneo ya vijijini ndani ya Tanzania Bara zinapata huduma ya maji safi na salama. Aidha, RUWASA inawajibika kutoa huduma za maji katika maeneo maalumu ya mijini kwa maelekezo ya Waziri mwenye dhamana ya sekta ya maji.

Huduma za maji katika maeneo ya vijijini husimamiwa na kuendeshwa na Vyombo vya Usimamizi wa Huduma za Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) chini ya usimamizi wa RUWASA katika ngazi ya Wilaya. Ili kuhakikisha uendelevu wa huduma za usambazaji maji, CBWSO hukusanya tozo za maji kutoka kwa jamii kama ilivyojadiliwa na kukubaliwa katika vyombo husika.

Aidha, CBWSO inawajibika katika kufanya matengenezo ya mradi ili kuhakikisha jamii inapata huduma ya maji safi na salama kila siku.