RUWASA ilirithi jumla ya skimu 1,379 za maji kutoka TAMISEMI. Kati ya hizo, skimu 177 zilikuwa na changamoto za utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi, skimu 1,202 zilikuwa zimekamilika.
Hadi kufikia Januari, 2024 RUWASA imefanya jitihadi kubwa za kukamilisha jumla ya skimu 159 kati ya 177 zilizokuwa na changamoto, Skimu 18 zipo katika hatua mbalimbali za ukamilishwaji.
Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 RUWASA imepanga kujenga jumla ya miradi ya maji 1,546
Kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023, RUWASA ilipanga kujenga miradi ya maji 1,029 ambapo kati ya hiyo miradi ya maji 630 imejengwa na kukamilika. i
Mikakati ya RUWASA kuhusu mapinduzi ya utoaji wa huduma ya maji hususani maeneo ya vijijini ni pamoja na:-
1. Ujenzi wa miradi ya maji yenye ubora na kujali thamani ya fedha.
2. Utoaji wa huduma ya maji kwa kutumia mita za malipo ya kabla ya matumizi (Prepaid Water Meter)