Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

RUWASA ni nini?

Majukumu ya RUWASA ni yapi?

Majukumu ya RUWASA yametajwa na kufafanuliwa katika kifungu cha 43 cha Sheria Na. 5 ya mwaka 2019 ya Huduma za Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira. Kwa ujumla,  RUWASA ina wajibu wa kuendeleza miundombinu kwa kufanya ujenzi na usimamizi wa ujenzi wa miradi ya maji na pia kusimamia utoaji wa huduma endelevu za maji na usafi wa mazingira vijijini. Katika kutekeleza jukumu hilo, RUWASA inafanya shughuli zifuatazo:-

· Kuandaa mipango, kusanifu miradi ya maji, kujenga na kusimamia uendeshaji wake.

· Kuendeleza vyanzo vya maji kwa kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi na kuchimba visima pamoja na kujenga mabwawa.

·  Kufanya matengenezo makubwa ya miundombinu ya maji vijijini.

· Kusajili, kuratibu, kudhibiti, kufuatilia na kutathmini vyombo vya kijamii vinavyohusika na uendeshaji wa huduma ya maji vijijini

    (Community Based Water Supply and Sanitation Organization - CBWSOs) ili kuhakikisha kuwa huduma inakuwa endelevu.

·  Kuzijengea uwezo CBWSOs kwa kutoa mafunzo na utaalamu wa uendeshaji na matengenezo ya miradi ya maji vijijini.

· Kuhamasisha jamii na kutoa elimu ya usafi wa mazingira katika ngazi ya kaya na mtu binafsi (sanitation and hygiene) na masuala ya

    uhifadhi na utunzaji wa vyanzo vya maji.

· Kutafuta fedha kwa ajili ya uendeshaji ili kuwezesha RUWASA kutekeleza majukumu yake na kushirikiana na wadau mbalimbali

    katika masuala yanayohusu utoaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira vijijini.

Chimbuko la RUWASA ni nini?

Je RUWASA inafanya kazi mpaka mikoani?

Katika ngazi ya Makao Makuu, RUWASA ina ofisi katika ngazi za Mikoa na Wilaya ambazo zinaongozwa na Mameneja wa Mikoa, na Mameneja wa Wilaya,na chini yao, kuna watumishi wa fani mbalimbali. Kwa sasa, RUWASA inafanyakazi katika Mikoa 25 kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Mkoa wa Dar es Salaam unahudumiwa na DAWASA katika maeneo yote na hivyo, haupo chini ya RUWASA.

Mipaka ya kiutendaji kati ya RUWASA na Mamlaka za Maji katika utoaji wa huduma ikoje?

●RUWASA inawajibika kutoa huduma katika maeneo ya vijinini na mijini ambayo hayahudumiwi na Mamlaka za Maji.

●Mamlaka za Maji zinawajibika kutoa huduma katika maeneo ya mijini au / na vijijini yaliyotangazwa na waziri mwenye dhamana na Sekta ya Maji.

●Katika maeneo ambayo hayajaundiwa Mamlaka za Maji huduma inatolewa kupitia Vyombo vya kijamii (CBWSOs)