Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Nini maana ya Chombo cha Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO)?

Nani anasajili Chombo cha Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii?

Chombo cha Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO) kinasajiliwa na Meneja wa RUWASA ngazi ya Wilaya baada ya Jumuiya hiyo kukidhi vigezo ya usajili. Vigezo vya Usajili vinapatika kwenye Sheria na Mwongozo wa Vyombo.

Nani anaweza kufuta usajili wa Chombo cha Watoa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO)?

Meneja wa RUWASA Wilaya anaweza kufuta usajili wa CBWSO endapo ataona haridhishwi na mwenendo wa uendeshaji wa mradi husika rejea kanuni No.829/05/11/2019, 21(1)

Nani anapanga bei za maji vijijini?

Bei za maji zinapendekezwa na Chombo husika kinachosimamia mradi kulingana na mwongozo wa upangaji bei za maji ulioandaliwa na RUWASA. Aidha, tozo ya maji huidhinishwa na Bodi ya RUWASA