Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI

"Maji Bombani"

Huduma za Usafi wa Mazingira

RUWASA kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu na OR-TAMISEMI kwa pamoja zina jukumu la kuhakikisha huduma za usafi wa mazingira zinazingatiwa na kutekelezwa katika maeneo ya vijijini. Hata hivyo, RUWASA inapaswa kuchochea na kuhamasisha jamii za vijijini kuzingatia usafi wa mazingira pamoja na kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji.

RUWASA inawajibika kutoa miongozo na kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya huduma za usafi wa mazingira maeneo ya vijijini.